KENYA: Gavana wa Kisumu asema uchaguzi hautarudiwa
Gavana wa kaunti ya Kisumu, magharibi mwa Kenya, amesema uchaguzi hautarudiwa katika jimbo hilo kama alivyotangaza mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC Wafula Chebukati Jumamosi.
Prof Anyang'a Nyong'o amesema kaunti hiyo itafanya maombolezi ya wiki moja kwa heshima ya watu wawili waliouawa leo.
"Nimetangaza kama gavana wa hii kaunti wiki moja ya maombolezi ambapo wakati huo hakutakuwa na sherehe. Kwetu uchaguzi huwa ni sherehe," amesema.
Amesema iwapo tume hiyo itaendelea kusisitiza uchaguzi ufanyike, basi wataenda kortini kutaka uzuiwe.
Comments
Post a Comment