Dk . Mashinji afunguka kilichojiri Ofisini kwa DCI

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji ameeleza kilichojiri kati yake na ofisa katika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Dk Mashinji amesema alichotarajia kukikuta kimekuwa tofauti.

"Awali nilikuwa na shaka kwamba wameniitia nini lakini kumbe ilikuwa ni majadiliano ya kawaida kati yangu na ofisi ya DCI," amesema Dk Mashinji leo Jumatano Oktoba 25,2017.

Amesema, "Majadiliano yalilenga kuelezana hiki kinachoendelea cha kamatakamata na je? sisi tunawaonaje na wao wanatuonaje. Pia, mambo mengine mengi."

Dk Mashinji amesema wamezungumzia pia kuhusu kuendelea kushikiliwa kwa Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Kigaila Benson.

Katibu mkuu Mashinji amesema ofisa huyo ameahidi kulifuatilia suala hilo.

"Mimi nimemweleza alichozungumza Kigaila kiko wazi na wala hakina tatizo lolote," amesema Dk Mashinji.

Comments

Popular posts from this blog

Faida ya kutumia ganda la Ndizi mbivu

Kurudisha nguvu za kiume

HISTORIA: Ernesto Guevara