Baada ya kuona ameolewa mume wake amejibu mapigo

Aliyekuwa mume halali wa muigizaji wa filamu bongo Irene Uwoya, mcheza soka kutoka nchini Burundi Hamad Ndikumana, ameonyesha kujibu mapigo baada ya mwenza wake kuonekana kuolewa, kwa kupost picha akiwa na mwanamke mwengine.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Ndikumana amepost picha hizo, huku akiandika ujumbe kama ambao unaonekana ni kurusha vijembe kwa mwenza wake huyo, ambaye hivi karibuni alimuandikia waraka kuanika yale aliyokuwa akithubutu kuyafanya, na kusema yuko tayari kutoa talaka.

Wawili hao walitfunga ndoa takatifu katika kanisa la Mtakatifu Joseph la Jijini Dar es salaam, na kutengana baada ya muda mfupi wa ndoa yao, huku kukiwa na tetesi kuwa hakuna maelewano baina yao.

Tazama mapicha aliyopost Ndikumana


Comments

Popular posts from this blog

Faida ya kutumia ganda la Ndizi mbivu

Kurudisha nguvu za kiume

Askari Aliyekuwa Akifanya Mapenzi na mfungwa ajinyonga