Alikiba akataa kuitwa Mungu wa Bongo fleva msiniite hivo siwezi kuwa hivo
Jinsi mashabiki wa soka wanavyochizika muda mwingine, ndivyo hivyo hata katika muziki. Kitu hiki kimemtokea shabiki mmoja wa Alikiba kitu kilichopelekea kumuita msanii huyo ‘Mungu wa Bongo Flava’.
Hata hivyo kilikuwa ni kitu ambacho hakikumpendeza Alikiba, ndipo alipoamua kumjibu shabiki huyo ambaye anatumia jina la Kibasalu katika mtandao wa Instagram;
Officialalikiba @kibasalu naomba msiniite hivyo siwezi kuwa wala siwezi kukubali imani yetu haturuhusu kujiita au kuitwa na mtu yoyote ule jina la MUUMBA.
Comment hiyo ya Alikiba inakuja mara baada ya shabiki huyo kwenda kwenye moja ya picha za msanii huyo katika mtandao wa Instagram na kuandika, ‘Bongo flaver god’.
Comments
Post a Comment