Tshishimbi amkuna Lwandamina Zanzibar

TSHISHIMBI. LICHA ya kiungo mpya wa Yanga, Papy Tshishimbi, kuchelewa kuanza kufanya mazoezi ya pamoja na wenzake, kocha wa klabu hiyo, Mzambia George Lwandamina, amesema amevutiwa na mwanzo wake mzuri na kufafanua kuwa atakuwa msaada kwao. Lwandamina alililiambia Nipashe jana kuwa, nyota huyo raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameonyesha kujituma katika mazoezi visiwani Zanzibar tangu alipojiunga rasmi na timu hiyo hivi karibuni. “Bado hana muda mrefu ndani ya kikosi, lakini kwangu naona ameanza vizuri na amekuwa mwepesi kushika maelekezo na kuzoea wenzake,” alisema Lwandamina bila kuweka wazi kama atamuanzisha mchezaji huyo kwenye mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Simba itakayopigwa Uwanja wa Taifa kesho.

Comments

Popular posts from this blog

Faida ya kutumia ganda la Ndizi mbivu

Kurudisha nguvu za kiume

Askari Aliyekuwa Akifanya Mapenzi na mfungwa ajinyonga