Miundombinu ya Gesi asilia kujengwa Dodoma , Mwanza, Tanga, Mbeya na Arusha

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania TPDC linakusudia kuanza utafiti wa namna ya usambazaji wa miundombinu ya kusafirishia gesi asilia kwenye mikoa ya Dodoma, Mwanza, Tanga, Mbeya na Arusha. Hatua hiyo inakwenda sambamba na kuandaa mpango kabambe wa mtandao wa miundombinu ya Gesi asilia mkoani Pwani ili kuwezesha viwanda vitakavyojengwa mkoani humo viweze kutumia gesi asilia. Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC Mhandisi KAPUULUYA MUSOMBA wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ziara ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iliyotembelea eneo la miundombinu ya gesi asilia na ufuaji umeme kwa kutumia gesi asilia lililopo Kinyerezi jijini Dar es salaam. Kwa upande wake serikali imebainisha nia yake ya kuhakikisha viwanda vingi nchini vinaunganishwa na matumizi ya gesi asilia ambapo hadi sasa viwanda 37 vimeshaunganishwa .

Comments

Popular posts from this blog

Faida ya kutumia ganda la Ndizi mbivu

Kurudisha nguvu za kiume

Askari Aliyekuwa Akifanya Mapenzi na mfungwa ajinyonga